Sunday, January 24, 2021

LAWAMA HUCHOCHEA HASIRA

 LAWAMA HUMFANYA MTU ASIJIREKEBISHE

Katika maisha tunayoishi watu wengi huwa wanatupa lawama kwa wengine kama matokeo yakija tofauti.


Hasa wenye mamlaka kama mzazi kwa mtoto,mwajiri kwa mwajiriwa n.k huwa wakifanya hivyo na badala ya mtu kukiri kosa huwa anajitetea sana na kuacha dosari kama ilivyokuwa.


Ikiwa umewahi kushuhudia matukio mbalimbali kutoka katika maisha ya kila siku utakuwa umeona hali hiyo.


Kuna mfano wa mhandisi mmoja alikuwa anasimamia ujenzi eneo fulani ambapo vibarua walipewa kofia za ngumu za  kujilinda dhidi ya vitu vikidondoka ili visiwadhuru.


Alikuja ghafla eneo la ujenzi akakutana na baadhi ya wafanyakazi hawajavaa kofia ngumu aliwafokea sana kwa tukio hilo.


Wakati anawafokea walivaa kofia zile huku walimsikiliza.


Alipomaliza kuwatofokea,kuwalaumu,kuwatishia aliondoka, ghafla vibarua wote walivua zile kofia hata wale waliokuwa wamevaa kwaa hiyari walizivua kwa hasira 


Waliamua kuzivua kwa sababu waliona wanapelekeshwa pamoja na kuwa ni kwa faida yao ila waliamua kufanya jeuri kwa kuona wanamkomoa.


Hali hiyo ipo kila sehemu.Mke akiunguza chakula na mume akianza kufoka,kutukana,kulaumu,kumtishia huwa anachochea kiburi kwa mke na mke hawezi kujirekebisha kwa kosa hilo badala yake atajitetea kuwa hakuwa na njia tofauti zaidi ya hiyo.


Na kwa sababu kiburi huwa kinakuja mtu akifokewa inapelekea akatae kosa badala yake ataweka visingizio kibao vya kufanya kosa husika .


Mtu huongozwa na mihemko ambapo akiwa mwenye hasira hufanya jeuri sana na akiwa mwenye furaha sana hufanya mambo ya ajabu ila akili ikiwa imetulia anafanya maamuzi mazuri.


Hata wewe ukifokewa,kutukanwa,kulaumiwa,kutishiwa huwezi kufanya kazi kwa weledi utafanya liwalo na liwe hata kumkomoa utafanya ikibidi.


Mfano mwajiri akimtukana mfanyakazi mbele ya wafanyakazi wengine kwa akili ya mwajiri atajua ametoa onyo kumbe karipio hilo limewaumiza walioshuhudia wote ambapo kila mmoja atakuwa anahofu siku ikiwa zamu yake.


Hofu hiyo itafanya wafanyakazi kufanya kazi kwa kufuata maagizo tu ili wasimuudhi mwajiri kwa kuepuka kutolewa,kutukanwa,kuvuliwa wadhifa katika ofisi.


Kila mtu anakuwa na hofu ya kuanzisha jambo ambalo mwajiri atakuwa hajalipitisha hivyo kukosekana kwa ubunifu kwenye ofisi.


Mtoto huwa anafurahi sana anapoonyeshwa tabasamu kutoka kwa mzazi wake ambapo humfanya ampende sana mzazi wake kupita kiasi.


Mtoto akifokewa,kutukanwa,kutishiwa,kupigwa,kudhalilishwa kwa kauli za ubaguzi wa rangi,kabila,lafudhi,muonekano,ufaulu duni au kukosea mara kwa mara humfanya mtoto kumuogopa mzazi na huwa anakuwa mzito sana kushirikiana na wengine kwa hofu ya kukosea.


Mtoto huanza kujibagua kwa rangi,lafudhi,kabila,muonekano,ufaulu kwa sababu amesikia kauli hizo mara kwa mara.


Mtoto akisifiwa sana kuwa yeye ni mzuri sana,mwenye akili sana,mcheshi sana,mwerevu sana huwa anajichukulia tofauti na watoto wanaoteswa


Mtoto anaepewa pongezi kwa kazi nzuri anazofanya,kupewa zawadi kwa juhudi,kuahidiwa kufanyiwa mambo mazuri akifanya vizuri huwa mwenye juhudi kuhakikisha anamfurahisha mzazi wake  kwa kuongeza juhudi katika kazi zake.


Mtoto anakatishwa tamaa,kukosolewa sana,kufokewa sana,kulaumiwa,kutuhumiwa uhalifu hata kama hajakosea huwa anakuwa mwenye hasira za kila wakati ambapo huwa hashauriki akiwa mkubwa kwa sababu kumchukulia kila mwenye mawazo tofauti kama adui kwa sababu tangu mtoto kila wazo lake lilipingwa vikali.


Mtu ambaye hawezi kupongeza juhudi za wafanyakazi waliopo chini yake huwa anafanya hivyo kwa sababu ya chuki,wivu,kisirani, kuhisi atapokonywaa cheo kama anayefanya vizuri atakubalika sana kumzidi.


Wapo watu kwenye ofisi akifika wafanyakazi huanza kujifanya wapo busy ili wasidhalilishwe mbele za wageni 


Ambao ni waajiri wenye uelewa huwa inakuwa rahisi kupewa ushirikiano kutoka kwa watu waliopo chini yake huku yule mwajiri mwingi wa lawama kila mtu humkimbia 


Ukiona wafanyakazi wenzio hawakuonyeshi ushirikiano ujue wewe ndiyo tatizo.


Kama unawatukana,kuwadhalilisha, kuwalaumu sana,hutoi pongezi mtu hata akifanya kazi nzuri kiasi gani,unakosoa kila juhudi za wafanyakazi,kuwaamini hata wafanyeje utaona hawakuonyeshi ushirikiano.


Kama unavyoona mtoto anapenda kupongezwa,kusifiwa,kupewa maneno laini hivyohivyo hata kwa watu wazima 


Mke alipopewa maneno laini,asiposifiwa kwa muonekano wake,upishi,juhudi,tabia zake huwa anajiona kama hayupo sehemu sahihi na huwa mwenye hasira sana utasikia 'mimi sina jema humu ndani kila ninapofanya kazi zozote lazima zitakosolewa na lawama juu'


Kama ni kazini mfanyakazi huongeza juhudi kama anasifiwa kwa kazi anazofanya kwa sababu binadamu atafanya juhudi ila asipopewa pongezi huanza kujitilia shaka kuhusu kazi zake anajiuliza kama anafanya kwa usahihi au anakosea.


Mtu unapomlaumu unafanya awe na kiburi,hasira,chuki,kisasi,wivu,kuweka vinyongo,kuanza kusengenya 


Hasira huwa inakuja kwa kila mtu hasa anapolaumiwa,kufokewa,kutukanwa,kudhalilishwa.


Wengine utasikia 'hivi kweli wewe umesoma? Chuo gani umesoma ambapo mnafundishwa ujinga kama huu?'


Hapo mtu huanza kupata hasira kwa sababu anaonekana hajasoma hata kama amesoma,kingine anajiona hafai,anajidharau,anapata hasira,anapata wivu,hasahau kauli hizo na huweza kubeba chuki na kutaka kulipa kisasi.


Wapo waliojiua kwa kukosolewa sana.


Kama wewe ni mtaalamu unapokosoa kazi zozote za watu tambua unaumiza hisia za watu hasa watu dhaifu ambao huamini uzuri wa kazi zao unatokana na maoni ya watu wengine.


Watu wanaojitambua huwa hawajali sana kauli mbaya za watu juu yao ila wengi ni dhaifu ambapo ukimkosoa tu tayari anaacha kile anachokifanya kwa hasira 


Mfano mtu anampelekea zawadi mama yake mzazi lakini mama yake mzazi hana shukurani badala mzazi ampongeza mwanae kwa zawadi ataanza kuikosoa sana zawadi hiyo jambo hilo humfanya mtoto kujichukia sana na ikiwa mzazi atasifia zawadi ya mtoto mwengine atafanya chuki kuenea baina ya watoto wake kwa kuanza kuonana kama maadui japo ni tumbo moja.


Wapo wazazi hubagua zawadi za watoto ambapo mtoto mmoja akimpa zawadi atasifia na mwengine ataikosoa  sana hata kama ni nzuri.


Kwa sababu binadamu huongozwa kwa hisia hufanya mgawanyiko kwa watoto ambapo huanza kuchukiana  wao kwa wao 


Hakikisha unajipenda sana hasa pale hakuna anaekuenda.


Jiamini sana hasa unapokosa mtu wa kukuamini 


Jijali sana hasa pale unapokosa mtu wa kukujali.


Tabasamu hata kama moyo wako unavuja damu.


Kupata kitabu cha

1.FIKRA ZAKO FURAHA YAKO (softcopy)

2TIBA YA MSONGO WA MAWAZO (hardcopy & softcopy)

3.BADILI FIKRA ZAKO BADILI MAISHA YAKO (hardcopy & Softcopy) 

4.MALEZI YA UBONGO KISAYANSI( hardcopy & softcopy)

 5.TABIA ZA WATU WALIOFANIKIWA (Hardcopy & softcopy)


6 MISINGI 10 YA FURAHA SIKU ZOTE (hardcopy &softcopy)


+255766862579

+255622414991


Imeandikwa na Psychologist

Said Kasege

Temeke,Dar es salaam

Wednesday, July 1, 2020

JE UNAWEZA KUMPONGEZA RAFIKI YAKO AKIKUZIDI KIPATO? Katika vitu huwanyima watu wengi raha ni pale akimwona mtu anaemjua au aliezaliwa nae sehemu moja au kusoma nae pamoja akiwa na muonekano mzuri kumzidi. Watu wengi huwa wanafurahi akiona wale alisoma nao au kuzaliwa nao mwaka mmoja anawazidi kipato na kama akiona wanamzidi anajenga chuki au wivu. Kisaikolojia kutokana na kuongezeka kwa matumizi ya mitandao ya kijamii hasa facebook,instagram kumefanya watu wengi kuishi kwa kushindana. Mtu hata kama amelala njaa ataweka picha ya miaka sita iliyopita ikimwonesha anakula chakula kizuri,kama akiwa na marafiki zake ataweka picha kuonesha anapendwa sana,kama akitembelea sehemu atahakikisha watu wote wamejua kama amesafiri,kama anafanya tukio lolote atahakikisha watu wote wanajua. Kwa muktadha huo imepelekea baadhi ya watu kuwajengea chuki ndugu zao au marafiki kwa kuamini wanawazidi kipato. Kisaikolojia watu wenye kujilinganisha na wengine ndio hupata Depression,stress na kuchanganyikiwa hasa anapotaka maisha ya watu wengine. Kwenye mitandao ya kijamii watu wengi huonesha maisha yenye mafanikio ili kuhakikisha anakuwa mwenye kusifika kulkko mwengine. Kitendo cha mtu kutaka kuonekana yupo juu kuliko wengine kinasababishwa na low self-esteem. Tatizo la low self-esteem hupelekea ushindani usiokuwa na maana.Mtu mwenye furaha huwa hashindani na watu wengine bali anashindana na yeye mwenyewe kuhakikisha leo yake ni bora kuliko jana. Ni kawaida watu wengi wakiona picha kwenye mitandao ya kijamii kutamani maisha ya wengine kwa kuona wao ni bora kumzidi. Katika utafiti uliofanywa nchini Marekani ilibainika kuwa watu wengi hufanya uigizaji (fake life) kwenye mitandao ya kijamii. Yupo mwanamitindo alikuwa analazimika kupiga picha akiwa na nguo za bei ghali sana,akiwa sehemu za kifahari si kwamba ndio maisha yake halisi bali alikuwa akitangaza biashara za watu. Alieleza kuwa aliamua kuacha kwa sababu anaishi maisha fake na kipato chake. Hali inakuwa mbaya zaidi kwa watu wa kipato cha chini ambao huwa wanaamini kila picha ya mtandaoni huku wakitamani maish ya wengine kuliko wao. Kisaikolojia hakuna binadamu mwenye sherehe kila siku. Kama unasumbuliwa na stress za ajira wengine wanazo pia za afya,uzazi,kusengenywa,kuteswa,kubaguliwa,hasara kwenye biashara,kufiwa ndugu zao,kuingia madeni,kufeli masomo,kufukuzwa kazi,kufeli usaili,kupoteza mali kwenye mikopo n.k kwa vyovyote usitamani maisha ya wengine kama ukijua maisha yao halisi na matatizo wanayopitia utafurahia maisha yako. Wewe mwenyewe ni shahidi wa matatizo unayopitia na kama utasema huna tatizo linalokukabili bila shaka wewe ndio tatizo lenyewe. Kamwe usidhani wengine wanafuraha kila siku bila huzuni si kweli. Kila mtu anamatatizo yake. Ndio sababu unatakiwa furaha yako ujipe mwenyewe. Kama hakuna anaekupenda jipende wewe Kama hakuna anaekuamini jiamini wewe. Utabaini kuwa hakuna binadamu utadumu nae siku zote. Kamwe usiweke mafanikio yako kwenye maamuzi ya mtu mwengine. Chanzo cha furaha yako ni wewe mwenyewe. Unaweza jitazama kwenye kioo kisha ukatamani sura yako baadhi ya viungo angepewa mwengine kama unafikra hizo unasumbuliwa na Low self-esteem Watu maarufu hawana sura za ajabu kuliko wewe isipokuwa wamejiamini na kupiga kazi kwa ubora wa hali ya juu bila kujali kasoro ambazo hawawezi kuzibadilisha. Watu wasiojiamini hutumia cosmetics,vyakula,mavazi kubadili muonekano ili wawavutie watu wasiowapenda. Mtu mwenye kukupenda hahitaji ujibadilishe bali anakupenda vile ulivyo. Kupata kitabu cha MALEZI YA UBONGO KISAYANSI NA MISINGI 10 YA FURAHA SIKU ZOTE.Piga +255766862579 +255622414991 Imeandikwa na Psychologist Said Kasege Temeke,Dar es salaam

WATU WASIOSHAURIKA

TAMBUA SIFA ZA WATU WASIOSHAURIKA
Wewe bila shaka ni mmoja kati ya watu ambao kuna tabia za ndugu,rafiki,mwajiri,mfanyakazi au yeyote unatamani aziache na haziachi na ulishajaribu kumpa ushauri na hashauriki na unakosa furaha kwasababu yake na hujui nini ufanye.

Leo nitakuorodheshea sifa za watu wasioshaurika.
Mtu asieshaurika anaweza kuwa yeyote msomi,asiekuwa msomi,kijana,mzee,mzazi au rafiki.

1.MTU ASIEKUBALI MAKOSA YAKE
wapo watu hawakubali makosa yao hata ukimkamata na ushahidi hakubali kosa.Shauri unavyoweza hutafanikiwa.

2.MTU MUONGEAJI SANA
huyu ni yule mwenye hasira za karibu na kitu kidogo ataongea sana kutwa nzima,huyu anaweza kuzusha ongemvi kidogo akalalamika sana na kuhadithia kila mtu.
Watu wenye tabia hizi ni wabishi wa hoja za wengine na ukiongea lolote anapinga hata kama hajui lolote.Ukichaa ni kupinga jambo ambalo hulijui ndani yake.

3.BLAME GIVER
Hawa ni wataalamu wa kulaumu wengine,mvua ikinyesha atalaumu,jua likiwaka atalaumu,lolote utasema atalaum.Ukimfanyia wema atatafuta dosari,ukimpigia simu atakulaumu kwa siku hukumtafuta awali,ukikaa kimya atalaumu kwa sababu hujamtafuta kwa vyovyote vile atakuwa anaona kasoro kwako.Watu hawa huwa akikwazana na mtu kazini anapeleka ugomvi kwa ndugu au wanafamilia yake kuwalaumu,kama biashara haina wateja atalaumu ndugu zake.chochote kinachomtokea atalaumu na watu hawa huwa na jazba sana,kauli zao ni kama vile utanambia nini umezaliwa nakuona,huwa wakali sana,wanaamini wakifa hakuna wa kuziba pengo,huwa wanapenda wakudhalilishe mbele za watu,wanakukejeli mbele za watu,huwa hawatunzi siri,huwa wanakusema vibaya watu hawa shauri mpaka utoke povu hawashauriki.

4.MJUAJI SANA
Hawa wanajua kila kitu ukianzisha mada atadakia kabla hujaimaliza ataongea anachojua,wasiokusikiliza ,mtu anaetumia simu ukianza kuongea,mtu anaetaka kukutawala huwezi kumshauri,mtu anaekutabiribia mabaya huwezi kumshauri,mtu anaeamini anajua kila kitu,mtu ambaye ukiongea anatafuta dosari akukosoe badala  ya kuzingatia ujumbe,mtu mwenye hasira sana,mtu anehoji kwa jazba,mtu anaetumia silaha kwenye mabishano huwa hawashauriki,mtu anaekudharau huwezi kumshauri,mtu aneamini hujui huwezi kumshauri,mtu mwenye kiburi huwezj kumshauri.

5.CHRONIC GOSSIP
Huyu ni mbea sana,ukimwambia jambo utalisikia kwa majirani huwezi kumshauri,mtu mwenye kupigana mafumbo au vijembe huwezi kumshauri.
Watu ambao unaogopa kuwatania kwa kuhofia watapokeaje utani huo huwezi kuwapa ushauri.

Kupata kitabu cha MALEZI YA UBONGO KISAYANSI na MISINGI 10 YA FURAHA SIKU ZOTE

+255766862579
+255622414991

Imeandikwa Na Psychologist
Said Kasege
Temeke,Dar es salaam

KUKATA TAMAA

MAUMIVU YA KUKATALIWA NA KUFELI
Hakuna mtu hajakataliwa na hakuna mtu hajafeli.
Wapo watu hujisifu kuwa hawajawahi kufeli na hupenda watu wawasifie kwa kufanya kwao vitu bila kufeli.

Kuna aina 2 za watu Introvert na Extrovert.
Introvert ni wapole,wenye upendo sana wanafikiri kwanza kisha wanaongea,wanahuruma sana,hawana hasira,hawakati tamaa haraka,hawapendi makuu,huwa wavumbuzi wa vitu vyao wenyewe,hufurahia upweke.

Extrovert hawa ndio wengi duniani ambao sifa zao ni kama kuongea kwanza kisha wanafikiria,wanapenda sana mikusanyiko,hupenda show off,huwa wanapata furaha kwa vitu au watu wengine ,hawawezi kudhibiti hasira zao,huwa waongeaji sana,huwa wanapenda makuu.

Watu wapole wakifeli hawakati tamaa ila wenye hasira hukata tamaa haraka.
Watu wapole hawana makuu kama kupelekesha wafanyakazi,kudhalilisha wenza wao,huwa na mapenzi ya dhati,huwa wanatunza siri,huwa wagumu kuanzosha uhusiano kwa sababu huwa hawaamini watu kirahisi,huwa wanaweza kucheza na watoto kwa urahisi huku wakali wakiwa wanapenda kutawala wengine,hupenda kubadili tabia za wengine,hupenda visasi,mafumbo,kejeli.

Maumivu ya kukataliwa ni sawa na maumivu ya kupigwa na kitu mwilini.Ukifeli au kukataliwa unaweza kupata hasira sana na mtu akipata hasira kwa kufeli au kukataliwa huwa akili haifanyi kazi na maamuzi yoyote mtu akifanya kwa hasira ni mabovo na hupelekea tatizo kuliko suluhu.

Ukifeli au kukataliwa si dhambi bali tafuta njia mpya ya kujaribu,jaribu tena,tena,tena mpaka ufanikiwe usiangalie umefeli mara ngapi angalia mara ngapi hujafanya.

Watu wenye hasira za karibu hawawezi kujaribu mara nyingi zaidi wakifeli kwa sababu hupenda mafanikio ya kulala na kuamka.Watu wenye hasira huwa wanazijua njia nyingi zitakazofanya ufeli kuliko njia moja itakayo kufanya ufaulu.

Ukiwa na watu waliokata tamaa kisha ukataka wakupe ushauri watakukatisha tamaa kwa sababu wao wenyewe wamekata tamaa.

Watu wapole hawalipi kisasi.Watu wenye hasira wanaweza kumhukumu mtu kwa taarifa za kusikia bila uchunguzi.
Wangapi wanawachukia watu maarufu ambao hawajawahi hata kuwaona?
Jibu ni wengi kwa sababu wao kila taarifa wakipewa wanaamini hata uchunguzi hawafanyi.

Watu wenye hasira hawajifunzi kwa sababu huwa wanapinga hoja hata kama hawajui lolote juu ya hoja hio.

Watu wapole huwa wanauliza sana maswali ili wajifunze huku wenye hasira huuliza ili wakuoneshe wanajua kukuzidi.

Hasira zinaweza kuzuia mafanikio yako kwa kiwango kikubwa.

85% ya mafanikio yako yanatokana na tabia zako huku 15% ni ujuzi uliosomea.
Mtu akiwa na kiburi kwa sababu amesoma maana yake anajivunia 15% halafu kwenye tabia anakuwa amefeli.

Watu hawapendi kuishi na wenye kiburi kwa sababu kila binadamu hupenda aoneshwe upendo ni ngumu sana mtu mwenye kiburi kuwapenda wengine.

Ukikataliwa kwako ni fursa ya kukubaliwa kwengine.Kama umepoteza fursa nyingi sana amini fursa zingine nzuri zipo njiani kwa ajili yako.
Ukikataliwa na mtu wa kwanza nenda kwa mwengine,mwengine,mwengine usiangalie wangapi wamekukatalia utakata tamaa bali angalia wangapi hujawafuata.

Dunia hii ina watu bilion 7.8 huwezi kumkosa mtu mwenye fikra kama zako.
Watu wenye kukupa msaada huchelewa kuja kwa sababu hio ndio maana unahusiwa uvumilivu na kutokata tamaa.

Watu hukata tamaa kwa kukosa uvumilivu.Watu wanakosa uvumilivu kwa sababu ya hasira,watu wanahasira kwa sababu wanataka mafanikio ya kulala na kuamka.

Usiweke mafanikio ya kulala na kuamka utakata tamaa.

Watu wanakukatalia si kwa sababu wewe ni mbaya au wanakuchukia hapana wanakukataa kwa sababu zao wenyewe.

Kamwe usifikiri watu watakupenda kwa sababu zako lah watu wanakupenda kwa sababu zao wenyewe na wanakuchukia kwa sababu zao wenyewe.

Jiamini tambua kabisa huwezi kufanikiwa bila kufeli au kukataliwa.
Acha wakukatae,kubali matokeo hata kama mabaya anza upya nafasi unayo sababu tu upo hai kila kitu kitaenda vema.

Kupata kitabu cha
MALEZI YA UBONGO KISAYANSI NA
MISINGI 10 YA FURAHA SIKU ZOTE

+255766862579
+255622414991

Imeandikwa na Psychologist
Said Kasege
Temeke,Dar es salaam

MOTISHA KWA WATU WENYE KUKATA TAMAA

MOTISHA :MOTISHA SEHEMU YA 2
Tupo kwenye ulimwengu wenye matatizo mengi sana na suluhu za matatizo zipo ila wachache wanazijua.

Hakuna mtu asiekuwa na matatizo hata kama ataonekana kwenye mitandao akitabasamu kamwe usitamani maisha yake.

Kila mtu ni shahidi wa nafsi yake.Hakuna asiehitaji kufika hatua moja mbele au zaidi.

Kama unahitaji usogee walau hatua moja bila shaka kipo kitu kimekuzuia kufika hapo unapotaka ndio sababu kila mtu anahitaji motisha.

Kama mtu hajui anataka nini ndio njia yeyote ataenda.
Maumivu ni sehemu ya maisha ya binadamu.

Kila unaemuona amefanikiwa siku moja alikuwa kama wewe au chini zaidi yako.

Tofauti ni kwamba hawajakata tamaa.Lazima utakataliwa hata uweje lazima baadhi ya watu watakukatalia maombi yako.Hata uwe mzuri kiasi gani wapo watu wataona ubaya wako hata ufanyeje.

Hata uwe na huruma vipi wapo watu watasema unaroho mbaya.

Hata uwapende watu wote duniani wapo watu watakuchukia kisirisiri au kwa wazi.

Haijalishi unamaadui kiasi gani,hainalishi huna "connections",haijalishi huna pesa ya kula,haijalishi umepata ajali,haijalishi unafedheheka,haijalishi unamagonjwa sugu miaka nenda rudi huponi,haijalishi biashara zako haziingizi faida,haijalishi unafanyiwa figisu ufukuzwe kazi,haijalishi umetelekezwa na baba yako au mama yako,haijalishi kwenu hakuna  mwenye kukusaidia,haijalishi kazi zote ulizotuma maombi umekataliwa,haijalishi umekosa mkopo wa masomo,haijalishi unalala chini,haijalishi hujasoma,haijalishi unatoka wapi jambo muhimu upo hai.

Haijalishi huna mtoto miaka nenda rudi,haijalishi unateswa na mama mkwe ,haijalishi ndugu wa mke au mume wanakuchukia na figisu wanakufanyia bado upo hai unaweza kufanya mabadiliko ya maisha yako.

Kamwe usikate tamaa.Kukata tamaa ndjo utakuwa umekubali kupoteza ushindi.
Kamwe usirudi nyuma.
Wapo watakukatisha tamaa ziba masikio.

Haijalishi kazi yako ni dhalili,haijalishi kazi yako kipato kidogo,haijalishi kazi yako unanyanyaswa,haijalishi kazi yako haina faida kubwa kwa sababu tu inakupa chakula basi inuka songambele.

Haijalishi ajira wanapata wengine we unakosa,haaijalishi umeachwa kwa kukksa pesa bado upo hai,inuka sogea hatua.

Sogea hata hatua moja hata kama huoni matokeo sogea,sogea,sogea utafanikiwa hata kwa kuchelewa.

Usimue roho kwa kuona wengine wanapata pesa kukuzidi,usiumie kuona wengine mambo yao yanaenda wewe hayaendi kama hnavyotarajia sogea hatua moja.

Kama watu wote wamekugeuka wewe sogea hatua moja,sogea,inuka,inuka tena,inuka tena mpaka ufike kwenye lengo.

Hata kama matokeo ni dhaifu sogea,sogea,hata kama maumivu ni makali sana sogea hatua moja,kamwe usikate tamaa hata kama watu wote wamekata tamaa juu yako wewe usikate tamaa.

Kupata kitabu cha MOTIVATION chenye jina BADILI FIKRA ZAKO BADILI MAISHA YAKO

Simu
+255766862579
+255622414991

Imeandikwa na Psychologist
Said Kasege
Temeke,Dar es salaam

Monday, August 14, 2017

said kasege is new blog designed to connect all youth and adults for the better life expectation
we are all human being have to unite to discuss different issues that concerning our lives and we would successed in one way or another .
my brothers and sisters have to come up all together to formulate good policy that would ensure our live could grow up to the maxmum point that in one way or another we may have better direction

i would like also to invite all people who are able to make a changes in our future expectation  may follow saidikasege@gmail.com 

we have to change our mind right now so that we could reach the point of success in this year 2017